Dodoma. Katibu
Wizara ya Viwanda na Biashara Prof. Riziki Shemdoe amewataka wafanyakazi wa
Wizara hiyo kufanya kazi kwa bidii, weledi na uadilifu ili kuyafikia matarajio
ya Mhe. Rais John Pombe Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa
kati unaotegemea Viwanda ifikapo mwaka 2025.
Akizungumza na watumishi hao kwa mara ya kwanza tangu alipoteuliwa
kuwa Katibu Mkuu Prof. Shemdoe alimshukuru Mhe Rais kwa kumuamini na kumteua na
kumuona anafaa kuongoza Wizara hiyo,
Prof. Shemdoe aliwataka watumishi kumpa ushirikiano wa kutosha
katika utendaji wa kazi kama walivyoonesha ushirikiano kwa Katibu Mkuu mstaafu.
“Hii ni wizara iliyobeba ajenda ya serikali ya awamu ya tano ya kuifanya nchi
yetu kuwa ya viwanda ili kukuza uchumi na kuchochea maendeleo ya watu hivyo tujue
sisi tumepewa jukumu kubwa ambalo tunapaswa kufanya ili wizara hii itoe matokeo
yanayotarajiwa na Mhe. Rais Magufuli. “Nawahakikishia kuwapa ushirikiano
na wakati wote ofisi yangu itakuwa wazi bila kikwazo chochote muda wote
nitapatikana nitakapohitajika.
Akielezea matarajio yake kwa watumishi hao Prof. Shemdoe aliwataka
kusimamia ajenda ya Tanzania ya Viwanda na pia anatarajia kuwa watafanya kazi
kwa uharaka na ufanisi.
Naye Katibu Mkuu aliyemaliza muda wake Prof. Joseph Buchweishaija
alimpongeza Prof. Shemdoe kwa kuteuliwa kuongoza Wizara hiyo.
“Nampongeza Prof. Shemdoe kwa kuteuliwa kuongoza Wizara hii, hii
ni wizara yenye watu wanaojituma na kufanya kazi kuanzia uongozi wa juu hadi
wafanyakazi wa chini”.
Akimkaribisha mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Bw. Ludovick Nduhiye
alieleza kuwa lengo la kikao hicho ni kufahamiana na kutambuana na alihaidi
kufanyika kwa kikao kingine cha kujadili mambo mbalimbali ya kiutendaji na
changamoto za watumishi.
Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi (TUGHE) Wizara ya Viwanda
alielezea kuhusu umuhimu wa baraza la wafanyakazi katika kupitisha bajeti ya
Wizara.
“Ulidokeza kuhusiana na maandalizi ya bajeti ya Wizara,
Tunatakiwa kupata wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi, tunarajia mwezi huu wa pili
kamishina wa kazi atakuja kwa ajili ya kufanya uchaguzi ili baade baraza hilo
liweze kupitisha bajeti ya Wizara kama ilivyo utaratibu”.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki
Shemdoe akisalimiana na kaimu mkurugenzi idara ya maendeleo ya Viwanda ndugu Leo Lyayuka mara baada ya kuwasili katika ofisi za wizara Mtumba jijini Dodoma.
| Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu wa wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki Shemdoe na watumishi katika ofisi za wizara Mtumba, jijini Dodoma. |
Katibu Mkuu Wizara ya
Viwanda na Biashara, Prof. Riziki Shemdoe akisaini kitabu katika ofisi yake
Mtumba, jijini Dodoma.
| Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Joseph Buchweishaija akikabidhi ofisi kwa Katibu mkuu mteule Prof. Riziki Shemdoe katika ofisi za wizara Mtumba, jijini Dodoma. |
![]() |
Katibu Mkuu Wizara ya
Viwanda na Biashara, Prof. Riziki Shemdoe akizungumza na wafanyakazi katika
ukumbi wa chuo kikuu cha Dodoma.
![]() |
Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano
wizara ya viwanda na biashara akiongoza mkutano kati ya Katibu mkuu wa wizara
ya viwanda na watumishi wa wizara kilifanya katika ukumbi wa chuo cha UDOM.
![]() |
Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof.
Joseph Buchweishaija akizungumza wakati wa kuwaaga watumishi wa wizara ya
viwanda na biashara.
![]() |
Picha ya pamoja ya Katibu mkuu wizara ya
viwanda na watumishi wa wizara hiyo.
![]() |
Baadhi ya watumishi wa wizara wakimsikiliza
kwa makini Katibu mkuu Prof. Shemdoe.




