Search This Blog

Thursday, December 17, 2020

Waziri wa Viwanda na Biashara afanya kikao na Menejimenti ya wizara, wakuu wa taasisi na wafanyakazi jijini Dodoma.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geoffrey Mwambe (Mb) amewaagiza Wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara kutengeneza taarifa ya mawasilisho ya majukumu watakayoyafanya kwa mwaka huu wa fedha.

Pia ametoa siku saba (7) kwa taasisi hizo kupeleka kwake ukomo wa bajeti na mikakati ya tofauti waliojiwekea kwaajili ya kuendeleza na kuleta mabadiliko katika taasisi hizo.

Waziri Mwambe ametoa maagizo hayo Jijini Dodoma wakati alipokutana na wakuu wa taasisi zilizochini ya Wizara, Wakuu wa idara na wafanyakazi ambapo amesema kila taasisi ihakikishe imeweka mikakati mipya ya kuleta mabadiliko katika sekta ya Viwanda na biashara. 

"Ndani ya siku saba (7) kila taasisi itengeneze taarifa na iwasilishwe kwangu juu ya mikakati mikubwa ya kufanyakazi na kuleta mabadiliko makubwa, kila taasisi ilete mikakati yake kujua imepanga kufanya nini" amesema Mhe. Mwambe.

Ametaka kila kitengo katika Wizara hiyo kujitafakari wanafanyaje kazi na wamejipangaje katika kuleta mabadiliko makubwa katika sekta yao ili kuimarisha sekta ya Viwanda na biashara iweze kulinufaisha taifa. 

Aidha ametaka watumishi hao kuwa wabunifu katika nafasi zao za kazi na kutengeneza kitu cha tofauti katika utumishi wao utakaoleta mabadiliko chanya katika sekta ya Viwanda na biashara hapa nchini.

Pia amezitaka taasisi hizo kutengeneza mifumo mipya ya utafutaji wa masoko ya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini ili bidhaa zinazotengenezwa hapa nchini zipate masoko ya ndani na nje ya nchi.


"Tuanze kutafuta masoko ya bidhaa zetu kuna wajasiliamali wanatengeneza bidhaa lakini hawana masoko hawa tunawakatisha tamaa, lakini akizalisha bidhaa na akapata soko inampa nguvu kuendelea kuzalisha zaidi"

 

"Tuwe wabunifu kuna kiwanda nilikitembelea kinazalisha maziwa lakini vifungashio wanafuata Kenya, namuuliza anasema hapa nchini hakuna, nikapita kiwanda kingine wanatengeneza vifungashio vilevile nae anasema hana soko hapa tunafanya uzembe hatuwauganishi hawa wazalishaji" amesema Mhe Mwambe.

Amesema kwa Sasa kuna masoko makubwa ya nje ya nchi ya bidhaa ambapo zinapatikana hapa nchini tena kwa wingi ni wajibu wa taasisi zinazohusika kuhamasisha wananchi kuzalisha bidhaa hizo na kutafuta masoko hayo.

Ameonya baadhi ya watumishi wa taasisi na Wizara kuwa kikwazo cwa kuchelewesha majibu ya maombi ya wafanyabiashara wanapotaka huduma.

"Unakuta mtumishi wa TBS anashirikiana na mshindani wa muomba vibali huyu kila akileta maombi ya kuthibitishwa anaambiwa hajakidhi viwango kumbe wewe unazunguka upande wa pili unachukua fedha" amesema.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud Kigahe (Mb), amewataka watumishi wa Wizara hiyo na taasisi zake kufanyakazi kwa ushirikiano ili kuleta matokeo chanya katika Wizara hiyo."Nataka mshirikiane muwe wamoja mtekeleze majukumu yenu kwa uadilifu na kuwa kiunganishi imara kati ya wafanyabiashara, wakulima na masoko ya bidhaa zao" amesema Mhe. Kigahe.


Waziri wa Viwanda na Biashara Mheshimiwa Geoffrey Mwambe akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo alipokutana nao Jijini Dodoma kuweka mikakati ya pamoja namna ya kuendeleza wizara hiyo na kuleta matokeo chanya.


Naibu Waziri wa Viwanda na biashara Mheshimiwa Exaud Kigahe akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo( hawapo pichani) wakati wa kikao cha Waziri wa Viwanda na biashara Mheshimiwa Geoffrey Mwambe, alipokutana nao Jijini Dodoma kuweka mikakati ya pamoja namna ya kuendeleza wizara hiyo na kuleta matokeo chanya.


Baadhi ya Watumishi mbalimbali wa Wizara ya Viwanda na biashara wakimsikiliza Waziri wa Viwanda na biashara Mheshimiwa Geoffrey Mwambe (hayupo pichani) walipokutana na Waziri wa Wizara hiyo Jijini Dodoma kuweka mikakati ya pamoja namna ya kuendeleza wizara hiyo na kuleta matokeo chanya.


Friday, December 11, 2020

Waziri na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara wawasili katika ofisi za wizara Mtumba na kupokelewa na Menejimenti pamoja na watumishi wa wizara.

 

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geofrey Idelphonce Mwambe (Mb) na Naibu Waziri wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Silaoneka Kigahe (Mb) leo tarehe 10 Desemba, 2020 wameripoti katika ofisi za wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma na kupokekewa na Menejimenti ya Wizara hiyo ikingozwa na Katibu Mkuu Prof Riziki Shemdoe na Naibu Katibu Mkuu ndugu Ludovick Nduhiye.

Wakizungumza na Menejimenti hiyo baada ya kufika ofisini hapo wote kwa pamoja wameomba ushirikiano mkubwa kutoka kwa Watumishi wote wa wizara huku wakisisitiza weledi na kujituma kwenye kazi kwa kila mmoja ndio siri ya mafanikio.

Akizungumza katika kikao kifupi na watendaji hao, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mwambe amewataka watumishi wote wa Wizara ya Viwanda kuumpa ushirikiano na kufanya kazi kwa kutumia taaluma zao na kuhaidi kufanya kikao kingine na wafanyakazi wote ili kujua changamoto  mbali mbali zinazowakabili watumishi na kuzifanyia kazi.

"Tunashukuru kwa mapokezi yenu yaliyojaa upendo, tunawaahidi ushirikiano, tutafanya vikao na taasisi zetu zote 15 zilizo chini ya wizara na kuzungumza na Wakurugenzi wakuu wa taasisi na pia wakuu wa Idara na vitengo" Alisema Mhe. Mwambe.

Aidha Mhe. Mwambe aliwataka wakuu wote wa Idara zinazosimamia taasisi hizo kuhakikisha zinaleta tija kwa Taifa letu na watanzania kwa ujumla.

Kwa upande wake Naibu Waziri, Mhe. Exaud Silaoneka Kigahe (Mb) amewaomba watumishi wote wa wizara hiyo kumpa ushirikiano kwa kuwa yeye  ni mwenyeji katika Wizara hiyo na kuwataka watumishi  wawe tayari kuendana na mabadiriko yalitokea na kuahidi kuwa atafanya kazi kwa weredi bila kumuonea mtu wala kuumpendelea mtu.

"Niwaombe tushirikiane kama Timu ili tuweze kufika tunapopataka, kwenye sekta zetu hizi yapo mambo ambayo yaliahidiwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa kuomba kura kwa wananchi na yapo kwenye Ilani ya CCM, ni kazi yetu kwenda kuyasimamia na kuyatekeleza kama yalivyoelekezwa" Alisema Mhe. Kigahe.

Nae Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Prof. Riziki Shemdoe amewapongeza Mawaziri kwa kuteuliwa kwao na kuwakaribisha huku akihaidi kutoa ushirikiano wa dhati kwa viongozi hao katika kuijenga Tanzania ya Viwanda.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geofrey Idelphonce Mwambe (Mb) pamoja na Naibu waziri Mhe. Exaud Kigahe (Mb) baada ya kupokelewa na Katibu wa wizara Prof. Riziki Shemdoe pamoja na Naibu Katibu Ludovick Nduhiye na watumishi wa wizara.

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geofrey Idelphonce Mwambe (Mb) akisalimiana na wafanyakazi wa wizara mara baada ya kuwasili katika ofisi za wizara zilizoko Mtumba jijini Dodoma.



Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geofrey Idelphonce Mwambe (Mb) akisaini katika ofisi za wizara Mtumba na kufanya majadiliano na Naibu waziri pamoja na Katibu Mkuu pamoja na Naibu Katibu Mkuu.


Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geofrey Idelphonce Mwambe (Mb) pamoja na Naibu waziri Mhe. Exaud Kigahe (Mb) wakipokea zawadi ya ukaribisho kutoka kwa mtumishi wa wizara Bi. Stella Nswima mara baada ya kufika katika ofisi za wizara Mtumba jijini Dodoma.


Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...