Search This Blog
Thursday, April 1, 2021
Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara
Thursday, December 17, 2020
Waziri wa Viwanda na Biashara afanya kikao na Menejimenti ya wizara, wakuu wa taasisi na wafanyakazi jijini Dodoma.
Pia ametoa siku saba (7) kwa taasisi hizo kupeleka kwake ukomo wa
bajeti na mikakati ya tofauti waliojiwekea kwaajili ya kuendeleza na kuleta
mabadiliko katika taasisi hizo.
Waziri Mwambe ametoa maagizo hayo Jijini Dodoma wakati alipokutana na wakuu wa taasisi zilizochini ya Wizara, Wakuu wa idara na wafanyakazi ambapo amesema kila taasisi ihakikishe imeweka mikakati mipya ya kuleta mabadiliko katika sekta ya Viwanda na biashara.
"Ndani ya siku saba (7) kila taasisi itengeneze taarifa na iwasilishwe kwangu juu ya mikakati mikubwa ya kufanyakazi na kuleta mabadiliko makubwa, kila taasisi ilete mikakati yake kujua imepanga kufanya nini" amesema Mhe. Mwambe.
Ametaka kila kitengo katika Wizara hiyo kujitafakari wanafanyaje kazi na wamejipangaje katika kuleta mabadiliko makubwa katika sekta yao ili kuimarisha sekta ya Viwanda na biashara iweze kulinufaisha taifa.
Aidha ametaka watumishi hao kuwa wabunifu katika nafasi zao za kazi na kutengeneza kitu cha tofauti katika utumishi wao utakaoleta mabadiliko chanya katika sekta ya Viwanda na biashara hapa nchini.
Pia amezitaka taasisi hizo kutengeneza mifumo mipya ya utafutaji
wa masoko ya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini ili bidhaa zinazotengenezwa hapa
nchini zipate masoko ya ndani na nje ya nchi.
"Tuanze kutafuta masoko ya bidhaa zetu kuna wajasiliamali
wanatengeneza bidhaa lakini hawana masoko hawa tunawakatisha tamaa, lakini
akizalisha bidhaa na akapata soko inampa nguvu kuendelea kuzalisha zaidi"
"Tuwe wabunifu kuna kiwanda nilikitembelea kinazalisha maziwa lakini vifungashio wanafuata Kenya, namuuliza anasema hapa nchini hakuna, nikapita kiwanda kingine wanatengeneza vifungashio vilevile nae anasema hana soko hapa tunafanya uzembe hatuwauganishi hawa wazalishaji" amesema Mhe Mwambe.
Amesema kwa Sasa kuna masoko makubwa ya nje ya nchi ya bidhaa ambapo zinapatikana hapa nchini tena kwa wingi ni wajibu wa taasisi zinazohusika kuhamasisha wananchi kuzalisha bidhaa hizo na kutafuta masoko hayo.
Ameonya baadhi ya watumishi wa taasisi na Wizara kuwa kikwazo cwa kuchelewesha majibu ya maombi ya wafanyabiashara wanapotaka huduma.
"Unakuta mtumishi wa TBS anashirikiana na mshindani wa muomba
vibali huyu kila akileta maombi ya kuthibitishwa anaambiwa hajakidhi viwango
kumbe wewe unazunguka upande wa pili unachukua fedha" amesema.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Exaud Kigahe (Mb), amewataka watumishi wa Wizara hiyo na taasisi zake kufanyakazi kwa ushirikiano ili kuleta matokeo chanya katika Wizara hiyo."Nataka mshirikiane muwe wamoja mtekeleze majukumu yenu kwa uadilifu na kuwa kiunganishi imara kati ya wafanyabiashara, wakulima na masoko ya bidhaa zao" amesema Mhe. Kigahe.
Friday, December 11, 2020
Waziri na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara wawasili katika ofisi za wizara Mtumba na kupokelewa na Menejimenti pamoja na watumishi wa wizara.
Waziri wa Viwanda na
Biashara Mhe. Geofrey Idelphonce Mwambe (Mb) na Naibu Waziri wa Wizara ya
Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Silaoneka Kigahe (Mb) leo tarehe 10 Desemba,
2020 wameripoti katika ofisi za wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma na
kupokekewa na Menejimenti ya Wizara hiyo ikingozwa na Katibu Mkuu Prof Riziki
Shemdoe na Naibu Katibu Mkuu ndugu Ludovick Nduhiye.
Wakizungumza na Menejimenti
hiyo baada ya kufika ofisini hapo wote kwa pamoja wameomba ushirikiano mkubwa kutoka
kwa Watumishi wote wa wizara huku wakisisitiza weledi na kujituma kwenye kazi
kwa kila mmoja ndio siri ya mafanikio.
Akizungumza katika kikao
kifupi na watendaji hao, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mwambe amewataka
watumishi wote wa Wizara ya Viwanda kuumpa ushirikiano na kufanya kazi kwa
kutumia taaluma zao na kuhaidi kufanya kikao kingine na wafanyakazi wote ili
kujua changamoto mbali mbali zinazowakabili
watumishi na kuzifanyia kazi.
"Tunashukuru kwa
mapokezi yenu yaliyojaa upendo, tunawaahidi ushirikiano, tutafanya vikao na
taasisi zetu zote 15 zilizo chini ya wizara na kuzungumza na Wakurugenzi wakuu
wa taasisi na pia wakuu wa Idara na vitengo" Alisema Mhe. Mwambe.
Aidha Mhe. Mwambe aliwataka
wakuu wote wa Idara zinazosimamia taasisi hizo kuhakikisha zinaleta tija kwa
Taifa letu na watanzania kwa ujumla.
Kwa upande wake Naibu
Waziri, Mhe. Exaud Silaoneka Kigahe (Mb) amewaomba watumishi wote wa wizara
hiyo kumpa ushirikiano kwa kuwa yeye ni mwenyeji
katika Wizara hiyo na kuwataka watumishi
wawe tayari kuendana na mabadiriko yalitokea na kuahidi kuwa atafanya
kazi kwa weredi bila kumuonea mtu wala kuumpendelea mtu.
"Niwaombe tushirikiane
kama Timu ili tuweze kufika tunapopataka, kwenye sekta zetu hizi yapo mambo
ambayo yaliahidiwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa
kuomba kura kwa wananchi na yapo kwenye Ilani ya CCM, ni kazi yetu kwenda
kuyasimamia na kuyatekeleza kama yalivyoelekezwa" Alisema Mhe. Kigahe.
Nae Katibu Mkuu wa Wizara
ya Viwanda na Biashara Prof. Riziki Shemdoe amewapongeza Mawaziri kwa kuteuliwa
kwao na kuwakaribisha huku akihaidi kutoa ushirikiano wa dhati kwa viongozi hao
katika kuijenga Tanzania ya Viwanda.
![]() |
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geofrey Idelphonce Mwambe (Mb) pamoja na Naibu waziri Mhe. Exaud Kigahe (Mb) baada ya kupokelewa na Katibu wa wizara Prof. Riziki Shemdoe pamoja na Naibu Katibu Ludovick Nduhiye na watumishi wa wizara.
![]() |
| Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geofrey Idelphonce Mwambe (Mb) akisalimiana na wafanyakazi wa wizara mara baada ya kuwasili katika ofisi za wizara zilizoko Mtumba jijini Dodoma. |
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Geofrey Idelphonce Mwambe (Mb) akisaini katika ofisi za wizara Mtumba na kufanya majadiliano na Naibu waziri pamoja na Katibu Mkuu pamoja na Naibu Katibu Mkuu.
Sunday, November 15, 2020
Nchi ya Tanzania yang'ara katika maonesho ya Kitamaduni nchini China.
Wanafunzi wa Tanzania wanaosomea Jiangxi, wameshiriki Maonesho ya Kitamaduni ya Kimataifa International Cultural Festival (ICF) yaliyofanyika tarehe tarehe 14 Novemba, 2020 nchini China.
Maonesho hayo ambayo hufanyika
mara moja kwa mwaka yalifadhiliwa na Chuo Kikuu cha Jiangxi cha masuala ya
Fedha na Uchumi (JUFE) ambapo yaliwakutanisha wanafunzi wanaoziwakilisha nchi
zao, wafanyabiashara na raia mbalimbali wa nchini China.
Katika maonesho hayo wanafunzi
wa Tanzania waliweza kuonesha fursa za uwekezaji na biashara katika bidhaa za
Korosho, Utalii, mapishi ya chakula cha asili cha Tanzania na madini ya
Tanzanite ambapo banda la Tanzania lilikuwa ni miongoni mwa vivutio kutokana na
maandalizi yake ambapo lilihusisha utalii wa Tanzania kwa kuonesha picha za
video na vipeperushi vilivyotolewa na ubalozi wa Tanzania nchini China.
Katika maonesho hayo kundi
la wanafunzi wanaosomea Uzamili kutoka Tanzania ambao pia ni watumishi wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiongozwa na afisa biashara
kutoka wizara ya Viwanda na Biashara ndugu, David Geofrey walishiriki kuandaa
banda la Tanzania.
Wanafunzi wa kitanzania wanasoma nchini China katika picha ya pamoja waliposhiriki maonesho ya Kitamaduni ya Kimataifa International Cultural Festival (ICF).
![]() |
| Bango likionesha vivutio mbalimbali vinavyopatikana nchini Tanzania. |
Raia wa China wakiwa katika banda la Tanzania kuona vivutio mbalimbali vinavyopatikana nchini Tanzania katika maonesho ya Kitamaduni ya Kimataifa International Cultural Festival (ICF).
Tuesday, October 20, 2020
Kikao cha menejimenti ya wizara kwa ajili ya kupitia sera ya viwanda vidogo na biashara ndogo, ukumbi wa chuo kikuu cha kilimo cha Sokoine (SUA) Morogoro.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki Shemdoe, leo tarehe 20 Oktoba, 2020 ameiongoza menejimenti ya wizara katika kikao kazi cha kujadili mapitio (Background paper) ya sera ya viwanda vidogo na vya kati ya mwaka 2003.
Katika kikao hicho kilichohudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu ndugu Ludovick Nduhiye, wakuu wa Idara na Vitengo kutoka wizara ya viwanda na biashara, wawakilishi kutoka sekta binafsi (TPSF), Taasisi mbalimbali za serikali pamoja na wadau wa maendeleo nchini ambao ni Mfuko wa Kuendeleza Sekta ya Fedha Tanzania (FSDT).
Prof. Shemdoe amesema
kwamba wizara imedhamiria kutunga sera za kuwawezesha wajasirimali wadogo
kuendeleza biashara ambapo katika blue print tozo mbalimbali ziliondolewa kwa
lengo la kuboresha mazingira bora ya wafanyabiashara. Hivyo katika sera hii
itawezesha wajasiliamali kufanya shughuli zao kwa urahisi pia uhakika wa mitaji
na mikopo.
Naye Mkuu wa Chuo Kikuu cha
Kilimo cha Sokoine (SUA) Prof. Raphael Chibunda ameipongeza wizara kwa maamuzi
ya kuchagua eneo la SUA kwa ajili ya kikao kazi hicho pia amesema shughuli za
kilimo zinaenda sawia na uendelezaji wa viwanda ambayo ndio ajenda ya nchi hii, hivyo basi ili viwanda vizalishe bidhaa za kutosha ni lazima malighafi za kilimo ziwe za kutosha kukidhi viwanda vyetu, Prof. Chibunda alisema pia sera hiyo itasaidia wakulima wanaojishughulisha na uzalishaji wa mazao ya kilimo
kuwezeshwa katika mitaji na mikopo nafuu kuendeleza shughuli zao.
Mapitio ya sera ya viwanda vidogo na biashara ndogo yaliwasilishwa na mtaalamu mwelekezi ambaye ni Dkt. Josephat Kweka na kupokea maoni ya kuboresha maeneo mbalimbali kutoka kwa menejimenti ya wizara na wadau waliohudhuria kikao kazi hiki.
Katibu
Mkuu Prof. Riziki Shemdoe akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya wizara
mara baada ya ufunguzi wa kikao kazi cha mapitio ya sera ya Viwanda vidogo na
biashara ndogo katika ukumbi wa chuo cha SUA, MOROGORO.
Baadhi ya wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na wadau mbalimbali waliohudhuria kikao kazi cha mapitio ya sera ya Viwanda vidogo na biashara ndogo |
TAARIFA KWA UMMA - TANZIA
SALAMU ZA POLE
20 Oktoba, 2020 - Dodoma
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa anatoa salamu za pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki kufuatia kifo cha Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Prof. Damian M. Gabagambi aliyefariki dunia leo tarehe 20 Oktoba, 2020 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam.
“Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya msiba wa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Natambua mchango wake mkubwa katika kuendeleza Sekta ya Viwanda na Biashara hapa nchini”.
Mhe. Bashungwa ametoa pole kwa menejimenti na wafanyakazi wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na wadau wote wa viwanda na biashara hapa nchini.
“Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana libarikiwe”
Monday, October 12, 2020
Uzinduzi wa Kiwanda cha kuchakata Pamba cha chama kikuu cha Ushirika (KACU LTD).
Naibu Katibu Katibu Mkuu, Lodovick Nduhiye, tarehe 8 Oktoba, 2020 Ameshiriki uzinduzi wa Kiwanda cha kuchakata pamba cha chama kikuu cha Ushirika (KACU LTD) Kilichopo wilaya ya Kahama.
Katika ufunguzi huo Naibu Katibu Mkuu alipata fursa ya kutoa saamu za wizara kwa kupongeza chama cha ushirika kwa hatua hiyo waliyofikia ya kuwa na Vinu vya kuchambulia pamba (ginnery) ambavyo vitasaidia katika kazi kuchambua pamba na kuongeza uzalishaji.
Aidha ameupongeza uongozi wa Kiwanda kwa juhudi kubwa wanazofanya kwani kwa hatua hiyo waliyofikia watasaidia ajira kwa watanzania wenzetu wa Kahama na mikoa ya jirani.
![]() |
| Naibu Katibu Mkuu Ludovick Nduhiye akitoa salamu za Wizara katika hafla ya ufunguzi wa kiwanda cha kuchakata pamba cha Chama Kikuu cha Ushirika (KACU LTD) kilichopo Wilaya ya Kahama. |
Prof. Shemdoe atembelea kiwanda cha Nellkanth Chemical L.t.d kilichopo eneo la Amboni jijini Tanga.
Katibu Mkuu wizara ya viwanda na biashara Prof. Riziki Shemdoe ametoa wito kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza nchini waje katika mkoa wa Tanga kwani yapo maeneo mengi ya kuwekeza katika sekta viwanda.
Wito
huo aliutoa jana alipotembelea kiwanda cha Nellkanth Chemical L.t.d kilichopo
eneo la Amboni jijini Tanga wakati alipofanya ziara ya siku moja.
Prof.
Shemdoe alisema kuwa Tanzania inavutia zaidi katika uwekezaji na maeneo
mengi ya uwekezaji yapo na yanatekelezwa kwa ajili yao hivyo kuwataka
wawekezaji wanaohitaji waje kuwekeza ili walipe kodi, walete ajira na mambo
mengine yanayoendana na uwekezaji.
“Wito
wangu kwa wawekezaji wengine waje wawekeze Tanzania, waje wawekeze mkoa wa
Tanga kuna maeneo mengi sana na magodauni ambayo yapo kwa sasa na yangeweza
kutumika kwa ajili ya viwanda, waje wakijua hapa nchini tuna blue print ambayo
inatekelezwa kwa ajili ya wawekezaji ili waje walipe kodi na kuleta ajira kwa
wananchi wetu” alisema.
Aidha
alizungumzia suala la uzalishaji katika kiwanda hicho na kusema kuwa kiwanda
hicho kina maeneo makubwa yanayofaa kuwekeza biashara zaidi ya uzalishaji
uliopo wa chokaa kwani wana maeneo mengine zaidi ya ekari 2,500 ambayo wanaweza
kulima chumvi ambayo imeshaanza kuonekana.
“Eneo
hili zamani lilikuwa halilimiki hapa lakini sasa kuna migodi ambayo inatoa
madini ambayo inazalishwa na kuleta faida nchini kwani wanalipakodi na kusaidia
wananchi kupata ajira, vilevile kuanzishwa kwa shamba hili kutatufanya sisi kuacha
kuagiza bidhaa hiyo kutoka nje ya nchi” alibainisha.
Hata
hivyo alisema kuwa kiwanda hicho kimefanya kazi kubwa kutokana na uzalishaji
wake kwani wameajiri wananchi zaidi ya 2,000 ambao wako kiwandani hapo na
wengine takribani 4,000 wako kwenye maeneo mengine ambayo yanamilikiwa na
mwekezaji huyo.
Naye
Mkurugenzi mzalendo wa kiwanda hicho Rashid Amour (Liemba) alisema kuwa kupitia
uzalishaji mkubwa wa kiwanda hicho tayari wameshateka masoko katika nchi
mbalimbali za Afrika mashariki na Maziwa makuu ambapo wamekuwa wakipeleka
bidhaa zao katika masoko ya ushindani.
“Kwakweli
mpaka sasa hivi soko letu kubwa liko Congo, lakini siyo Congo pekeyake bali
tumeziteka nchi za Kenya, Burundi, Rwanda na Uganda, kwa sasa hivi bidhaa yetu
tunashukuru tumezishika nchi zote za Afrika mashariki maana wao ndiyo
wanapambana na sisi” alifafanua Liemba.
“Kama
mnavyofahamu biashara ni ushindani na sisi tumeingia kwenye ushindani na nchi
hizi, tunaiomba serikali iweze kutusaidia katika ushindani huu na kama
itatusaidia nina hakika ushindani huu tutaushinda bila matatizo” aliongeza.
Aidha
alieleza kwamba kwa sasa ushindani mkubwa wanaoupata ni kutoka nchi ya Afrika
kusini ambako pia alizungumzia hofu yake kuhusu soko hilo kwamba nchi ya Congo
imeshaingiliwa na nchi ya China ambayo inatengeneza bidhaa hiyo ya chokaa
kupeleka huko.
“Kwa
sasa hivi ushindani wetu mkubwa uko South Africa kwa Congo, sasa hivi Congo
wameingia wachina, wachina wanajitahidi sana kutengeneza bidhaa kuleta hapa nao
ni chokaa kama sisi na mpaka sasa hivi tunajitahidi kupambana nao”
aliongeza.
Hata
hivyo alibainisha kwamba kiwanda hicho kinapambana katika soko la chokaa lakini
zipo biashara nyingine wanazozalisha kama vile magnissium (MGO) ambavyo vyote
vinatumika kusafishia cooper ambapo pia alitoa takwimu ya bidhaa
wanazosafirisha kupeleka kwenye masoko nje ya nchi.
“Congo
peke yake tunapeleka siyo chini ya tani elfu kumi lakini kipindi cha nyumba
tulikuwa tunakwenda mpaka tani elfu ishirini, Kenya na Zambia nako pia
tunapeleka tani kumi vilevile kwahiyo ni tani elfu ishirini kwa mwezi”
alifafanua.
![]() |
| Katibu Mkuu Prof. Riziki Shemdoe akipokea maelezo ya kiwanda cha Nellkanth Chemical L.t.d alipokitembelea kusikiliza changamoto za kiwanda hicho katika ziara yake ya kutembelea Viwanda Mkoani Tanga. |
Wednesday, September 30, 2020
Mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya Rushwa.
Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu ndugu Issa Ng'imba afungua mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya rushwa kazini yaliyofanyika leo tarehe 30 Septemba, 2020 katika ukumbi wa Makao makuu ya jeshi la zima moto na Uokoaji, Dodoma.
Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi na kupinga rushwa mahala pa kazi katika kuwahudumia wananchi.
Mafunzo hayo ya siku moja yamehudhuriwa na watumishi wa Wizara kutoka idara na Vitengo.
![]() |
Mkurugenzi wa Idara
ya Utawala na Rasilimali watu ndugu Issa
Ng'imba akifungua mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na
mapambano dhidi ya rushwa kazini leo tarehe 30 Septemba, 2020 |
Thursday, September 24, 2020
Mkutano kati ya Menejimenti ya Wizara na ujumbe kutoka Ubalozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Ally Gugu leo tarehe 24 Septemba, 2020 amekutana na ujumbe kutoka Ubalozi wa Afrika ya kusini nchini Tanzania katika ofisi za Wizara zilizopo mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.
Akiongea na ugeni huo, ndugu Ally Gugu alisema kuwa Tanzania na Afrika Kusini zimekuwa kwenye ushirikiano wa kibiashara, kiuchumi na kisiasa kwa muda mrefu tangu kipindi cha kudai uhuru. Hivyo ni jambo jema kushirikiana katika kuendeleza biashara kati ya nchi hizo mbili.
Alisema ushirikiano huo umezidi kuimarika kwa uwepo wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo nchi hizi mbili zilikubaliana kuwa na Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika Sekta ya Viwanda na Biashara. Lengo la MoU hiyo ni kuimarisha uhusiano wa kibiashara zaidi kwa kuongeza biashara (trade volume) kwa maslahi ya pande zote mbili ukizingatia Afrika ya Kusini ni moja ya nchi iliyokinara katika uwekezaji barani Afrika.
Naye Kaimu balozi wa Afrika ya Kusini, ndugu Sizwe Mayoli amesema
kuwa amefurahi kupata fursa ya kujadili masuala ya ushirikiano wa kiuchumi,
kibiashara na uwekezaji baina ya Tanzania na Afrika ya Kusini katika kikao
hicho.
Aidha, baadhi ya masuala yaliyojadiliwa katika kikao hicho ni pamoja na kupata taarifa ya hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Hati ya Makubaliano (MoU) ya Ushirikiano katika Sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji. MoU hiyo inatoa fursa ya kuunda Kamati ya Pamoja ya Biashara na Uwekezaji ktika nchi hizi mbili.
Pia kikao hiki kimehitimishwa kwa pande zote
mbili kuunda kamati ya pamoja itakayoshirikisha wajumbe kutoka Tanzania na Afrika
ya Kusini ili kushirikiana pamoja katika kutekeleza Hati ya makubaliano (MoU) katika
sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya
Viwanda na Biashara, Ally Gugu (wa kwanza kushoto) akizungumza wakati wa kikao
na Kaimu balozi wa Afrika ya Kusini, ndugu Sizwe Mayoli walipokutana leo tarehe
24 Septemba, 2020 katika ofisi za Wizara zilizopo mji wa Serikali Mtumba jijini
Dodoma, kushoto ni ndugu Dumo Siyotula katibu wa siasa wa ubalozi wa Afrika ya
kusini
............................................................................................................................................................
Imetolewa na:
Kitengo cha Habari na Mawasiliano,
Wizara ya Viwanda na Biashara,
24 Septemba, 2020
Thursday, September 3, 2020
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki S. Shemdoe Leo tarehe 3 Septemba, 2020 ameongoza kikao cha Kamati ya Uongozi (Steering Committee) ya Uwezeshaji Biashara.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki S. Shemdoe Leo tarehe 3 Septemba, 2020 ameongoza kikao cha Kamati ya Uongozi (Steering Committee) ya Uwezeshaji Biashara katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jijini Dodoma.
Lengo la kikao hiki
lilikuwa ni kujadili utekelezaji wa maelekezo ya mkutano wa kwanza wa kamati
hiyo uliofanyika tarehe 13 Februari 2020.
Masuala yaliyojadiliwa na
kuidhinishwa ni pamoja na hadidu za rejea (ToR) za kamati ya kitaifa ya uwezeshaji
biashara, Maeneo ya kundi A, B na C ya mkataba wa uwezeshaji biashara wa
Shirika la Biashara la Dunia (WTO TFA) ambayo yatawasilishwa sekretarieti ya
WTO kabla ya tarehe 22 Septemba, 2020.
Utekelezaji wa masuala
mengine ya biashara nje ya mkataba wa uwezeshaji biashara, utekelezaji wa mpango mwelekeo (Roadmap) wa miaka mitano
(2020/21 - 2024/2025) na mpango kazi (Action Plan) ya mwaka 2020/2021. Aidha,
Kamati imetoa maelekezo ya maboresho ya Mfumo wa taarifa za ufanyaji biashara
(National Trade Information Module) kabla ya kufanyiwa uzinduzi rasmi.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Mwinyi Talib Haji akizungumza wakati wa kikao cha kamati ya uongozi kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jijini Dodoma.
Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...


















