Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya
Viwanda na Biashara, Ally Gugu leo tarehe 24 Septemba, 2020 amekutana na ujumbe
kutoka Ubalozi wa Afrika ya kusini nchini Tanzania katika ofisi za Wizara
zilizopo mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.
Akiongea na ugeni huo,
ndugu Ally Gugu alisema kuwa Tanzania
na Afrika Kusini zimekuwa kwenye ushirikiano wa kibiashara, kiuchumi na kisiasa
kwa muda mrefu tangu kipindi cha kudai uhuru. Hivyo ni jambo jema kushirikiana
katika kuendeleza biashara kati ya nchi hizo mbili.
Alisema ushirikiano
huo umezidi kuimarika kwa uwepo wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika
(SADC) ambapo nchi hizi mbili zilikubaliana kuwa na Hati ya Makubaliano (MoU)
ya ushirikiano katika Sekta ya Viwanda na Biashara. Lengo la MoU hiyo ni
kuimarisha uhusiano wa kibiashara zaidi kwa kuongeza biashara (trade volume) kwa maslahi ya pande zote
mbili ukizingatia Afrika ya Kusini ni moja ya nchi iliyokinara katika
uwekezaji barani Afrika.
Naye Kaimu balozi wa Afrika ya Kusini, ndugu Sizwe Mayoli amesema
kuwa amefurahi kupata fursa ya kujadili masuala ya ushirikiano wa kiuchumi,
kibiashara na uwekezaji baina ya Tanzania na Afrika ya Kusini katika kikao
hicho.
Aidha, baadhi ya masuala yaliyojadiliwa katika
kikao hicho ni pamoja na kupata taarifa ya hatua iliyofikiwa katika utekelezaji
wa Hati ya Makubaliano (MoU) ya Ushirikiano katika Sekta ya Viwanda, Biashara
na Uwekezaji. MoU hiyo inatoa fursa ya kuunda Kamati ya Pamoja ya Biashara na
Uwekezaji ktika nchi hizi mbili.
Pia kikao hiki kimehitimishwa kwa pande zote
mbili kuunda kamati ya pamoja itakayoshirikisha wajumbe kutoka Tanzania na Afrika
ya Kusini ili kushirikiana pamoja katika kutekeleza Hati ya makubaliano (MoU) katika
sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya
Viwanda na Biashara, Ally Gugu (wa kwanza kushoto) akizungumza wakati wa kikao
na Kaimu balozi wa Afrika ya Kusini, ndugu Sizwe Mayoli walipokutana leo tarehe
24 Septemba, 2020 katika ofisi za Wizara zilizopo mji wa Serikali Mtumba jijini
Dodoma, kushoto ni ndugu Dumo Siyotula katibu wa siasa wa ubalozi wa Afrika ya
kusini
Baadhi ya wajumbe kutoka Wizara ya Viwanda
na Biashara pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
walioshiriki kikao hicho.
 |
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya
Viwanda na Biashara, Ally Gugu (kushoto) akizungumza na Kaimu balozi wa Afrika
ya Kusini, ndugu Sizwe Mayoli wakati wa kikao cha kujadili Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika
Sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji. |
............................................................................................................................................................
Imetolewa na:
Kitengo cha Habari na Mawasiliano,
Wizara ya Viwanda na Biashara,
24 Septemba, 2020