Search This Blog

Wednesday, September 30, 2020

Mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya Rushwa.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu ndugu  Issa Ng'imba afungua mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya rushwa kazini yaliyofanyika leo tarehe 30 Septemba, 2020 katika ukumbi wa Makao makuu ya jeshi la zima moto na Uokoaji, Dodoma. 

Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi na kupinga rushwa mahala pa kazi katika kuwahudumia wananchi.

Mafunzo hayo ya siku moja yamehudhuriwa na watumishi wa Wizara kutoka idara na Vitengo.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu ndugu Issa Ng'imba akifungua mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya rushwa kazini leo tarehe 30 Septemba, 2020


Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara walioshiriki mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya rushwa kazini yaliyofanyika katika ukumbi wa Makao makuu ya jeshi la zima moto na Uokoaji, Dodoma.

Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara walioshiriki mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya rushwa kazini yaliyofanyika katika ukumbi wa Makao makuu ya jeshi la zima moto na Uokoaji, Dodoma.

Thursday, September 24, 2020

Mkutano kati ya Menejimenti ya Wizara na ujumbe kutoka Ubalozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania.

 

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Ally Gugu leo tarehe 24 Septemba, 2020 amekutana na ujumbe kutoka Ubalozi wa Afrika ya kusini nchini Tanzania katika ofisi za Wizara zilizopo mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma.

Akiongea na ugeni huo, ndugu Ally Gugu alisema kuwa Tanzania na Afrika Kusini zimekuwa kwenye ushirikiano wa kibiashara, kiuchumi na kisiasa kwa muda mrefu tangu kipindi cha kudai uhuru. Hivyo ni jambo jema kushirikiana katika kuendeleza biashara kati ya nchi hizo mbili.

Alisema ushirikiano huo umezidi kuimarika kwa uwepo wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) ambapo nchi hizi mbili zilikubaliana kuwa na Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika Sekta ya Viwanda na Biashara. Lengo la MoU hiyo ni kuimarisha uhusiano wa kibiashara zaidi kwa kuongeza biashara (trade volume) kwa maslahi ya pande zote mbili ukizingatia Afrika ya Kusini ni moja ya nchi iliyokinara katika uwekezaji barani Afrika.

Naye Kaimu balozi wa Afrika ya Kusini, ndugu Sizwe Mayoli amesema kuwa amefurahi kupata fursa ya kujadili masuala ya ushirikiano wa kiuchumi, kibiashara na uwekezaji baina ya Tanzania na Afrika ya Kusini katika kikao hicho.

Aidha, baadhi ya masuala yaliyojadiliwa katika kikao hicho ni pamoja na kupata taarifa ya hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Hati ya Makubaliano (MoU) ya Ushirikiano katika Sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji. MoU hiyo inatoa fursa ya kuunda Kamati ya Pamoja ya Biashara na Uwekezaji ktika nchi hizi mbili.

Pia kikao hiki kimehitimishwa kwa pande zote mbili kuunda kamati ya pamoja itakayoshirikisha wajumbe kutoka Tanzania na Afrika ya Kusini ili kushirikiana pamoja katika kutekeleza Hati ya makubaliano (MoU) katika sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.


Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Ally Gugu (wa kwanza kushoto) akizungumza wakati wa kikao na Kaimu balozi wa Afrika ya Kusini, ndugu Sizwe Mayoli walipokutana leo tarehe 24 Septemba, 2020 katika ofisi za Wizara zilizopo mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, kushoto ni ndugu Dumo Siyotula katibu wa siasa wa ubalozi wa Afrika ya kusini

Baadhi ya wajumbe kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki kikao hicho.

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Ally Gugu (kushoto) akizungumza na Kaimu balozi wa Afrika ya Kusini, ndugu Sizwe Mayoli wakati wa kikao cha kujadili Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika Sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.


............................................................................................................................................................

Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano,

Wizara ya Viwanda na Biashara,

24 Septemba, 2020


Thursday, September 3, 2020

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki S. Shemdoe Leo tarehe 3 Septemba, 2020 ameongoza kikao cha Kamati ya Uongozi (Steering Committee) ya Uwezeshaji Biashara.

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Riziki S. Shemdoe Leo tarehe 3 Septemba, 2020 ameongoza kikao cha Kamati ya Uongozi (Steering Committee) ya Uwezeshaji Biashara katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jijini Dodoma.

Lengo la kikao hiki lilikuwa ni kujadili utekelezaji wa maelekezo ya mkutano wa kwanza wa kamati hiyo uliofanyika tarehe 13 Februari 2020.

Masuala yaliyojadiliwa na kuidhinishwa ni pamoja na hadidu za rejea (ToR) za kamati ya kitaifa ya uwezeshaji biashara, Maeneo ya kundi A, B na C ya mkataba wa uwezeshaji biashara wa Shirika la Biashara la Dunia (WTO TFA) ambayo yatawasilishwa sekretarieti ya WTO kabla ya tarehe 22 Septemba, 2020.

Utekelezaji wa masuala mengine ya biashara nje ya mkataba wa uwezeshaji biashara, utekelezaji wa  mpango mwelekeo (Roadmap) wa miaka mitano (2020/21 - 2024/2025) na mpango kazi (Action Plan) ya mwaka 2020/2021. Aidha, Kamati imetoa maelekezo ya maboresho ya Mfumo wa taarifa za ufanyaji biashara (National Trade Information Module) kabla ya kufanyiwa uzinduzi rasmi.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Mwinyi Talib Haji akizungumza wakati wa kikao cha kamati ya uongozi kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jijini Dodoma.

Katibu Mkuu, Prof. Riziki Shemdoe katika picha ya pamoja na wajumbe walioshiriki kikao cha kamati ya uongozi kilichofanyika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) jijini Dodoma.


Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...