Search This Blog

Wednesday, September 30, 2020

Mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya Rushwa.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu ndugu  Issa Ng'imba afungua mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya rushwa kazini yaliyofanyika leo tarehe 30 Septemba, 2020 katika ukumbi wa Makao makuu ya jeshi la zima moto na Uokoaji, Dodoma. 

Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi na kupinga rushwa mahala pa kazi katika kuwahudumia wananchi.

Mafunzo hayo ya siku moja yamehudhuriwa na watumishi wa Wizara kutoka idara na Vitengo.

Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu ndugu Issa Ng'imba akifungua mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya rushwa kazini leo tarehe 30 Septemba, 2020


Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara walioshiriki mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya rushwa kazini yaliyofanyika katika ukumbi wa Makao makuu ya jeshi la zima moto na Uokoaji, Dodoma.

Baadhi ya watumishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara walioshiriki mafunzo ya wadau kuhusu maadili ya utumishi wa umma na mapambano dhidi ya rushwa kazini yaliyofanyika katika ukumbi wa Makao makuu ya jeshi la zima moto na Uokoaji, Dodoma.

Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...