NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe.
Mhandisi STELLA MANYANYA (Mb), amesema kunahaja ya kuziwezesha kifedha taasisi
za utafiti zinazobuni na kutekeleza teknolojia rahisi hapa nchini ili kufikia
lengo la kuwa na viwanda na kufikia uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka
2025.
Naibu Waziri Manyanya ameyasema hayo jijini
Dodoma wakati akizindua teknolojia mpya ya mashine ya kukamua mchuzi wa zao la
zabibu katika kiwanda kidogo Cha WENDECHE kilichopo Kata ya Hombolo Bwawani,
iliyobuniwa na TEMDO kwa kushirikiana na SIDO.
Alisema kuna haja ya kuziwezesha taasisi kama
SIDO, TEMDO, CAMATEC, TIRDO na nyinginezo, kwani kwa muda mrefu taasisi hizo
zilikuwepo lakini hazikuweza kunufaisha Watanzania. Lakini tangu zimewezeshwa kifedha tayari matokeo
yameanza kuonekana.
"Hii inafurahisha sana hizi taasisi
zimewezsshwa na matokeo chanya tumeyaona, "alisema Manyanya.
Alisema kuwezeshwa kwa taasisi hizi pia
kumesaidia ukuaji wa viwanda nchini, na
inatia moyo kuviwezesha zaidi..
Aidha amewahimiza Watanzania kuthamini vitu
vinavyotengenezwa hapa nchini, ikiwamo kuthamini viwanda vidogo kwa sababu
vinasaidia kutoa ajira kwa Watanzania, huku akiitaka SIDO kuhakikisha inasimamia
wenye viwanda vidogo kuhakikisha wanapata mikopo kutoka benki ya kilimo
Tanzania, TIDB, ili kuviongezea nguvu.
Alisema hakuna haja ya kubaki nyuma tunafanya
kile tunachoweza na baadae kitaleta matokeo makubwa hapo baadae na kufikia
Tanzania ya viwanda kama ilivyokusudiwa na Serikali ya awamu ya tano
inayoongozwa na Mhe. Rais John P. Magufuli.
Alisema ni vema SIDO wakaweka jitihada ya
kuwa karibu na watu hao ambao wakiwezeshwa wanaweza kuleta matokeo chanya
katika kile ambacho wanafanya.
Mbali na hilo Naibu Waziri Manyanya amewapa
wiki tatu TEMDO kuhakikisha wanawatengenezea mashine wajasiriamali ambao
walitoa oda ya kutengenezewa mashine hiyo ili nao waendelee na shughuli ya
uchakataji wa zabibu kwani mashine hizo ni nzuri na zina ufanisi wa hali ya
juu.
Alisema hakuna sababu ya kuwacheleweshea kwa
sababu wanahitaji kwa ajili ya kufanya maendeleo.
Kwa upande wake Meneja Taasisi ya ubunifu na
uhandisi Mitambo, TEMDO, Mhandisi Alexander Komba, alisema kazi yao ni kubuni
na kuendeleza Technolojia kwa ajili ya wajasiliamali wazalishaji, kisha
kupeleka kwa SIDO ili ziweze kuwafikia walengwa. Kutokana na ushirikiano huo
taasisi hizo mbili ambazo ziko chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara, waliweza
kutatua changamoto ya kuchakata zao la Zabibu kwa haraka.
![]() |
| Muonekano wa mashine ya kuchakata mchuzi wa Zabibu iliyobuniwa na kutengenezwa na TEMDO kwa ushirikiano wa SIDO. |
![]() |
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhandisi Stellah
Manyanya,akiangalia waini zinazotengenezwa katika kiwanda kidogo Cha
WENDECE kilichopo Kata ya Hombolo Bwawani, Wilaya ya Dodoma.
|



