Search This Blog

Tuesday, October 20, 2020

TAARIFA KWA UMMA - TANZIA



SALAMU ZA POLE 


20 Oktoba, 2020 - Dodoma

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa anatoa salamu za pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki kufuatia kifo cha Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Prof. Damian M. Gabagambi aliyefariki dunia leo tarehe 20 Oktoba, 2020 katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam.

“Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya msiba wa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Natambua mchango wake mkubwa katika kuendeleza Sekta ya Viwanda na Biashara hapa nchini”.

Mhe. Bashungwa ametoa pole kwa menejimenti na wafanyakazi wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na wadau wote wa viwanda na biashara hapa nchini.

“Bwana ametoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana libarikiwe”                                        

Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...