Search This Blog

Monday, October 12, 2020

Uzinduzi wa Kiwanda cha kuchakata Pamba cha chama kikuu cha Ushirika (KACU LTD).

Naibu Katibu Katibu Mkuu, Lodovick Nduhiye, tarehe 8 Oktoba, 2020 Ameshiriki uzinduzi wa Kiwanda cha kuchakata pamba cha chama kikuu cha Ushirika (KACU LTD) Kilichopo wilaya ya Kahama.

Katika ufunguzi huo Naibu Katibu Mkuu alipata fursa ya kutoa saamu za wizara kwa kupongeza chama cha ushirika kwa hatua hiyo waliyofikia ya kuwa na Vinu vya kuchambulia pamba (ginnery) ambavyo vitasaidia katika kazi kuchambua pamba na kuongeza uzalishaji.

Aidha ameupongeza uongozi wa Kiwanda kwa juhudi kubwa wanazofanya kwani kwa hatua hiyo waliyofikia watasaidia ajira kwa watanzania wenzetu wa Kahama na mikoa ya jirani.

Naibu Katibu Mkuu Ludovick Nduhiye akitoa salamu za Wizara katika hafla ya ufunguzi wa kiwanda cha kuchakata pamba cha Chama Kikuu cha Ushirika (KACU LTD) kilichopo Wilaya ya Kahama.





Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...