Search This Blog

Sunday, December 8, 2019

Mhe. Bashungwa afanya mkutano na Wamiliki na Wasimamizi wa Viwanda cha Samaki Mwanza

Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Viwanda na Biashara akiongoza majadiliano kwenye kikao chake na Wamiliki na Wasimamizi wa Viwanda vya Samaki Jijini Mwanza 



MKUTANO WA WAMILIKI NA WASIMAMIZI WA VIWANDA VYA SAMAKI KANDA YA ZIWA  

Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Viwanda na Biashara leo Desemba 8, amekutana na kufanya kikao na wamiliki na wasimamizi wa viwanda vya samaki vilivyopo Kanda ya Ziwa Jijini Mwanza.
Kikao hicho ambacho pamoja na mambo mengine, kililenga kwenye kubaini changamoto mbalimbali zinazowakabili wenye viwanda na hatimaye kutafuta ufumbuzi wa pamoja na Serikali kiliandaliwa chini ya mwamvuli wa Chama cha Wasindikaji Samaki na Kampuni za Uvuvi za Viwandani yaani kwa Kiingereza, Tanzania Industrial Fishing and Processors Association (TIFPA).  
Baadhi ya changamoto na kero ambazo wadau hao walizibaini kuzuia maendeleo ya viwanda vya samaki nchini ni pamoja na usafirishaji wa bidhaa nje ya nchi na nyaraka za kuuza nje, marejesho ya kodi ya ongezeko la thamani (VAT) pamoja na ushuru mkubwa.
Mhe. Bashungwa yuko Jijini Mwanza kwa ziara ya kikazi ambapo anatarajia kutembelea viwanda vilivyopo Jijini humo, na kuzungumza na wafanyakazi ili kubaini changamoto zinazokabili viwanda vya ukanda wa Ziwa Victoria, vilivyopo Jijini humo.   

MWISHO
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Viwanda na Biashara,
08 Desemba, 2019





Mhe. Bashungwa akiwa kwenye picha ya pamoja na Wadau wa Viwanda vya Samaki Jijini Mwanza.  


Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...