Search This Blog

Friday, December 20, 2019

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara afungua mkutano wa mwaka wa TCCIA


Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Mhandisi Stella Martin Manyanya (Mb.) amefungua mkutano Mkuu wa mwaka wa TCCIA leo tarehe 20/12/2019 katika hotel ya four points ya Sheraton (zamani New Africa Hotel) jijini Dar es Salaam. 
Katika hotuba yake Mhe. Manyanya amewataka TCCIA kuwa chemba ya kutoa dira na kuwaongoza wanachama wake kusimama imara katika kujenga uchumi wa Viwanda. Pia amewataka kutekeleza mkakati wao mpya kwa uadilifu unaolenga kuimarisha TCCIA; kuhakikisha mahusiano mazuri na Serikali; na kuimarisha ofisi za Mikoa na Wilaya ziweze kutoka huduma bora zaidi.

Pichani Mhe. Eng. Stella Manyanya (Mb.) NWVB pamoja na viongozi wa TCCIA wakiwemo pia baadhi ya wawakilishi kutoka mashirika ya kimataifa na mabalozi waliohudhuria mkutano Mkuu wa Mwaka wa TCCIA uliofanyika tarehe 20/12/2019 jijini Dar es Salaam.

Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...