Search This Blog

Tuesday, December 10, 2019

WAZIRI BASHUNGWA AKUTANA NA MAKAMU MWENYEKITI WA CHAMA CHA KIKOMUNISTI CHA VIETNAM

Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Viwanda na Biashara akisalimiana na Mhe.Pham Minh, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Kikomunisti cha Vietnam leo tarehe 10.12.2019 


Mhe. Innocent Bashungwa Waziri wa Viwanda na Biashara leo tarehe 10 Desemba 2019, amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Kikomunisti kutoka Vietnam Mhe. Pham Minh na ujumbe wake kwenye Kituo cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo yao ambayo yalijikita kwenye misingi na umuhimu wa ushirikiano wa kidugu baina ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nchi ya Vietnam, Mhe. Bashungwa alitumia fursa hiyo kumshukuru mgeni huyo na Serikali ya Vietnam kwa kununua Korosho ya msimu 2018/2019 zaidi ya asilimia 70 ya mzigo uliokuwepo.

Naye Mhe. Minh, kwa upande wake aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kudumisha mahusiano mazuri hususan kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), ambacho ndio kinachoongoza Serikali nchini.

MWISHO





Viongozi wakiwa kwenye mazungumzo pamoja na wajumbe waliohudhuria wakifuatilia mazungumzo hayo. 

Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...