Search This Blog

Monday, December 30, 2019

Waziri Bashungwa aitisha kikao kufuatilia maelekezo yake kwenye Kiwanda cha Chai cha Kagera

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa leo tarehe 30.12.2019 ameongoza kikao cha ufuatiliaji wa maelekezo aliyoyatoa tarehe 19.12.2019 alipotembelea kiwanda cha Kagera Tea Company Ltd na Mashamba ya wakulima wa chai Mkoani Kagera.


Kikao hicho pia kimehudhuriwa na Mhandisi Stella Manyanya Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,  Mkurugenzi wa Kiwanda cha chai Kagera, na wadau wengine muhimu ukiwemo uongozi wa CRDB Bank, wawakilishi kutoka TSHTDA, OTR, TADB, TCB, TRIT. 
Kwenye kikao hicho Mhe. Waziri ameiagiza Bodi ya Chai Tanzania (TBT), TSHTDA, TRIT  kuwatembela wakulima wa chai ili kuwasaidia kulima chai kwa kiwango kizuri na chenye tija. Vilevile ameagiza iundwe kamati maalum itakayoshirikisha taasisi zote muhimu, kwenda kiwandani na kufanya uchambuzi wa uzalishaji wa kiwanda hicho na pia kuwatembelea wakulima wa chai ili kupata ripoti ambayo itawasidia wakulima kunufaika na kilimo. Ameipa kamati hiyo wiki mbili kukamilisha kazi hiyo na kuwasilisha ripoti ofisini kwake.

Pia amesema mwezi wa kwanza atavitembelea viwanda vya Mponde na Lupemba ili kutafuta mstaakabali mzuri wa viwanda viwanda vyote ya chai nchi.




Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...