Search This Blog

Thursday, December 12, 2019

Waziri Bashungwa afungua Kongamano la Wafanyabiashara wa Kanda ya Magharibi

Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Viwanda na Biashara akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Biashara Kanda ya Magharibi Mjini Shinyanga leo tarehe 12.12.2019


Mhe. Innocent Bashungwa Waziri wa Viwanda na Biashara amekuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Kongamano la Biashara na Wakandarasi wa Kanda ya Magharibi. Kongamano hilo lililoandaliwa na Benki ya CRDB limefanyikia katika Ukumbi wa Mikutano wa NSSF Shinyanga, Tarehe 12 Disemba 2019.
Kongamano hilo lililolenga kujadili na kubadilishana mawazo kuhusu bidhaa mbalimbali zinazotolewa na kubuniwa na Benki ya CRDB, limehudhhuriwa pia na viongozi wa mikoa ya kanda hiyo wakiwemo Mhe. Aggrey Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Mwandisi Robert Gabriel, Mkuu wa Mkoa Geita na Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga, Mkuu wa Mkoa Kigoma.
Washiriki wa kongamano hilo lililodhaminiwa na Benki ya CRDB kutoka mikoa ya Kanda ya Magharibi (Shinyanga, Tabora, Geita na Kigoma); walibainisha kuwa huduma zinazoendelea kubuniwa na kutolewa na Benki hiyo zimerahisisha upatikanaji wa mitaji na mikopo kwa Wafanyabiashara na Wakandarasi wa mikoa husika.
Akifungua rasmi Kongamano hilo, Mhe. Bashungwa amewasisitiza Wafanyabiasha, Wakandarasi na washiriki wote kuchamngamkia fursa iliyowekwa na Benki ya CRDB ili kukuza biashara zao na kupata faida zaidi. Alisema kwa kufanya hivyo fursa za ajira kwa vijana wa kanda hiyo zitaongezeka na hatimaye pato la Serikali kuongezeka kupitia ulipaji wa kodi.


MWISHO


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Viwanda na Biashara,
12 Desemba, 2019



Mhe. Aggrey Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora akitoa utangulizi kuhusu Kongamano hilo lililoandaliwa na Benki ya CRDB kwa ajili ya Wafanyabiashara na Wahandisi wa Kanda ya Magharibi

Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo lililofanyikia kwenye Ukumbi wa Mikutano wa NSSF Mjini Shinyanga tarehe 12.12.2019

Viongozi wakibadilishana mawazo baada ya Kongamano hhilo kufunguliwa 


Picha ya Pamoja

Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...