![]() |
| Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Viwanda na Biashara akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Biashara Kanda ya Magharibi Mjini Shinyanga leo tarehe 12.12.2019 |
Mhe. Innocent Bashungwa
Waziri wa Viwanda na Biashara amekuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Kongamano
la Biashara na Wakandarasi wa Kanda ya Magharibi. Kongamano hilo lililoandaliwa
na Benki ya CRDB limefanyikia katika Ukumbi wa Mikutano wa NSSF Shinyanga,
Tarehe 12 Disemba 2019.
Kongamano hilo lililolenga
kujadili na kubadilishana mawazo kuhusu bidhaa mbalimbali zinazotolewa na
kubuniwa na Benki ya CRDB, limehudhhuriwa pia na viongozi wa mikoa ya kanda
hiyo wakiwemo Mhe. Aggrey Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Mwandisi Robert
Gabriel, Mkuu wa Mkoa Geita na Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga, Mkuu
wa Mkoa Kigoma.
Washiriki wa kongamano hilo lililodhaminiwa
na Benki ya CRDB kutoka mikoa ya Kanda ya Magharibi (Shinyanga, Tabora, Geita
na Kigoma); walibainisha kuwa huduma zinazoendelea kubuniwa na kutolewa na
Benki hiyo zimerahisisha upatikanaji wa mitaji na mikopo kwa Wafanyabiashara na
Wakandarasi wa mikoa husika.
Akifungua rasmi Kongamano
hilo, Mhe. Bashungwa amewasisitiza Wafanyabiasha, Wakandarasi na washiriki wote
kuchamngamkia fursa iliyowekwa na Benki ya CRDB ili kukuza biashara zao na
kupata faida zaidi. Alisema kwa kufanya hivyo fursa za ajira kwa vijana wa
kanda hiyo zitaongezeka na hatimaye pato la Serikali kuongezeka kupitia ulipaji
wa kodi.
MWISHO
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Viwanda na Biashara,
12 Desemba, 2019
![]() |
| Mhe. Aggrey Mwanri, Mkuu wa Mkoa wa Tabora akitoa utangulizi kuhusu Kongamano hilo lililoandaliwa na Benki ya CRDB kwa ajili ya Wafanyabiashara na Wahandisi wa Kanda ya Magharibi |
![]() |
| Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo lililofanyikia kwenye Ukumbi wa Mikutano wa NSSF Mjini Shinyanga tarehe 12.12.2019 |
![]() |
| Viongozi wakibadilishana mawazo baada ya Kongamano hhilo kufunguliwa |
![]() |
| Picha ya Pamoja |





