Search This Blog

Tuesday, December 3, 2019

TAARIFA KWA UMMA


MKUTANO WA WAMILIKI WA VIWANDA VYA NYAMA NA NGOZI

Wizara ya Viwanda na Biashara inapenda kuwafahamisha wenye Viwanda vya Nyama, Ngozi pamoja na wadau wote wa sekta hiyo kuwa Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Viwanda na Biashara anatarajia kukutana na wadau wa sekta hiyo Alhamis tarehe 05 Desemba, 2019, kuanzia saa 5.30 asubuhi katika ukumbi wa Mikutano uliopo ofisi za Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC).
 Madhumuni ya mkutano ni kujadili mikakati mbalimbali ya Serikali inayowekwa kwa ajili ya maendeleo ya sekta hiyo na wadau husika.  Kwa maelezo zaidi wasiliana na Wizara, Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali.

MWISHO


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Viwanda na Biashara,
03 Desemba, 2019

Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...