Search This Blog

Sunday, December 15, 2019

Mnyororo wa Thamani wa Biashara ya Samaki Mwanza

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa alipata wasaa wa kutembea mitaani na kuingia mwaloni Mwanza kwa mguu kuangalia hali ya biashara hasa ya mnyororo wa thamani wa samaki aina ya sangara na kubadilishana mawazo na wafanyabiashara wadogo wa maeneo hayo na wavuvi. 

"Nimejifunza kwamba hakuna kinachotupwa, hadi uti wa
mgongo wa samaki unatumiwa kusagwa na kuchanganywa na chakula cha kuku. Ni muhimu kuweka mwalo katika hali ya usafi na kusimamia mnyororo wa thamani wa sangara kuhakikisha tunapata maximum value ya kumnufaisha mvuvi, mfanyabiashara na mapato ya Serikali"


Mhe. Bashungwa akiwa kwenye picha na wafanyabiashara ya samaki alipotembea kwa miguu sokoni humo ili kujionea mnyororo wa biashara ya samaki na mapato yanayopatikana  


Prof. Kitila Mkumbo aanza kazi muda mchache mara baada ya kuapiswa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akimuapisha Profesa Kitila Alexander Mkumbo kuwa Waziri wa Viwanda n...